MKUTANO MKUU WA 10 WA KAUKI

MKUTANO MKUU WA 10 WA KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

KAUKI-Kidamali, Iringa

KAUKI-Kidamali, Iringa
Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Friday, January 27, 2017

SHUKRANI KWA WANAUKOO - KANDA YA IRORE



Uongozi wa Umoja Wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI), kwa niaba ya Wana Ukoo wote, unawashukuru wote waliofanikisha Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI, uliofanyika Vilalo, Kanda ya Irore, Mkoani Iringa, tarehe 2 Julai 2016. Tunatambua kuandaa mkutano wowote ni gharama, hivyo tunawapongeza kwa kujitoa kwao. Ni shughuli inayohitaji raslimali watu, fedha na zana ili kuweza kufikia lengo. Ni jambo la kujivunia na pia kutia moyo kwa wale wote ambao wameshiriki kikamilifu na kwa hali na mali katika jukumu hili. Licha ya kuwepo kwa watu wachache walioshiriki katika maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI, lakini umeweza kufanyika kwa mafanikio.



KAUKI pia inatoa shukrani za pekee kwa Uongozi wa KAUKI Kanda ya Irore, kwa kuhamasisha Wana Ukoo kushiriki kikamilifu katika maandalizi na pia kushiriki katika Mkutano Mkuu wa 11 wa KAUKI. Shukrani za pekee ziwaendee Ndugu Castory Kivenule, Pius Kivenule, Benard Kivenule, Amalia Kivenule, Michael Mateka na Wanaukoo kwa ujumla kwa moyo wao wa upendo na ukarimu, kwa kuamua kubeba jukumu hili. Uongozi wa KAUKI unawashukuru pia wanaukoo wote toka Kanda nyingine za Kidamali, Dar es Salaam na Kalenga kwa ushiriki wao. Pengine, kutokuwepo kwao, Mkutano huo usingeweza kufanikiwa.

Mwisho, shukrani za pekee ziwaendee ndugu zetu walioshiriki Mkutano Mkuu wa 11 kwa mara ya kwanza. Hii inaonesha dhamira yao ya dhati ya kuendelea kushirikiana na Wana Ukoo wenzao. Hali kadhalika wameonesha shauku ya kutaka kuujua ukoo na kuwafahamu wenzao.

Asante,

Imeandaliwa na:

Adam Kivenule
Katibu Mkuu, KAUKI