MKUTANO MKUU WA 10 WA KAUKI

MKUTANO MKUU WA 10 WA KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

KAUKI-Kidamali, Iringa

KAUKI-Kidamali, Iringa
Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Monday, July 1, 2013

UCHAGUZI WA VIONGOZI WA KANDA WA KAUKI MWAKA 2013, KUFANYIKA



Kanda sita (6) za KAUKI zitakuwa katika mchakato wa kufanya uchaguzi wa
kanda zao, mara tu baada ya kumalizika kwa Mkutano Mkuu wa 9 wa KAUKI.
Mkutano huo ulielekeza kuwa Walezi wasimamie uchaguzi huo katika kanda
zao. Taarifa kuhusiana na uchaguzi huo zitawekwa katika kurasa za blogs and
facebook za KAUKI.
-        Kanda ya Magubike
  1. Mwenyekiti
  2. Katibu
  3. Mweka Hazina

-        Kanda ya Kidamali
  1. Mwenyekiti
  2. Katibu
  3. Mweka Hazina

-        Kanda ya Nduli
  1. Mwenyekiti
  2. Katibu
  3. Mweka Hazina

-        Kanda ya Irore
  1. Mwenyekiti
  2. Katibu
  3. Mweka Hazina

-        Kanda ya Mufindi
  1. Mwenyekiti
  2. Katibu
  3. Mweka Hazina

-        Kanda ya Dar es Salaam
  1. Mwenyekiti
  2. Katibu
  3. Mweka Hazina

1.      Kanda ya Magubike
  1. Kamati ya Mipango na Maendeleo
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Mahesabu na Fedha
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Nidhamu na Maadili
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Maafa na Matatizo
-        Mwenyekiti
-        Katibu

2.      Kanda ya Kidamali
  1. Kamati ya Mipango na Maendeleo
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Mahesabu na Fedha
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Nidhamu na Maadili
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Maafa na Matatizo
-        Mwenyekiti
-        Katibu

3.      Kanda ya Nduli
  1. Kamati ya Mipango na Maendeleo
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Mahesabu na Fedha
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Nidhamu na Maadili
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Maafa na Matatizo
-        Mwenyekiti
-        Katibu

4.      Kanda ya Irore
  1. Kamati ya Mipango na Maendeleo
-        Mwenyekiti
-        Katibu


  1. Kamati ya Mahesabu na Fedha
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Nidhamu na Maadili
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Maafa na Matatizo
-        Mwenyekiti
-        Katibu

5.      Kanda ya Mufindi
  1. Kamati ya Mipango na Maendeleo
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Mahesabu na Fedha
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Nidhamu na Maadili
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Maafa na Matatizo
-        Mwenyekiti
-        Katibu

6.      Kanda ya Dar es Salaam
  1. Kamati ya Mipango na Maendeleo
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Mahesabu na Fedha
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Nidhamu na Maadili
-        Mwenyekiti
-        Katibu
  1. Kamati ya Maafa na Matatizo
-        Mwenyekiti
-        Katibu

UCHAGUZI WA WALEZI WA KAUKI
Angalau Mlezi Mmoja atoke kila Kanda
-        Kanda ya Magubike
-        Kanda ya Kidamali
-        Kanda ya Nduli
-        Kanda ya Irore
-        Kanda ya Mufindi
-        Kanda ya Dar es Salaam


MKUTANO MKUU WA 9 WA KAUKI WAFANYIKA MAGUBIKE, IRINGA


Wahamishiwa Kijijini Magubike Kumuenzi Mzee Hussein Tavimyenda Kivenule

https://www.facebook.com/kivenule
Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI) umefanya Mkutano wake Mkuu wa 9 wa umoja huo katika eneo la Magubike. Mkutano huo ulifanyika siku ya Jumamosi eneo la Magubike tofauti na Kidamali, kama ilivyopangwa katika Mkutano Mkuu wa 8 wa KAUKI.

Sababu za msingi za kuhamishia Mkutano Magubike ilikuwa ni kumuenzi muasisi pekee ya Ukoo wa Kivenule aliyekuwa amebaki, ambaye aliaga dunia siku ya Jumatano ya tarehe 25 Juni 2013, katika hospitali ya Ipamba, iliyopo Iringa.

Kwa kuzingatia umuhimu wake kwa ukoo wa Kivenule na pia kumpa heshima, Uongozi wa KAUKI ulibadilisha mahali pa kufanyia Mkutano ikiwa ni muhsusi ya kuuheshimu mchango wake na juhudi kubwa aliyoifanya kuunganisha ukoo wa Kivenule.

Mzee Hussein Sigatambuli Tavimyenda Tagumtwa Kivenule, alizikwa siku ya Alhamisi katika makaburi yaliyopo eneo la Magubike, karibu kabisa na nyumbani kwake. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi, Amina.

Kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa 9 wa KAUKI, kulienda sambamba na kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa Viongozi wa KAUKI, ambao walikuwa wanamaliza muda wao. Uchaguzi huo uliwarudisha katika uongozi baadhi ya viongozi wake waliokuwa madarakani; akiwemo Katibu Mkuu Ndugu Adam Alphonce Sigatambule Tavimyenda Tagumtwa Kivenule, Makamu wa Mwenyekiti Ndugu Christian John Kivenule, Mweka Hazina Ndugu Justin Daniel Kivenule, Mweka Hazina Msaidizi Ndugu Caroline Sigatambule Kivenule na Jermana Peter Mhapa.

Baadhi ya washiriki wa Mkutano Mkuu wa 8 wa KAUKI uliofanyika Jijini Dar es Salaam, mwaka 2012
Hali kadhalika, Mwenyekiti Mwasisi wa KAUKI alirudishwa katika madaraka kwa kuchukua nafasi ya Mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Ndugu Donath Peter Mhapa. Mwenyekiti wa sasa wa KAUKI ni Ndugu Faustino Sigatambule Tavimyenda Tagumtwa Kivenule, ambaye makazi yake ni Kidamali.

Aliyekuwa Kiongozi wa Kanda ya Magubike Ndugu Vitus Nzala alichaguliwa kuwa Makamu wa Katibu wa KAUKI.

Ifuatayo ni safu ya viongozi wa KAUKI:
1. Mwenyekiti                     Ndugu Faustino Sigatambule Kivenule
2. Makamu Mwenyekiti         Ndugu Christian John Kivenule
3. Katibu Mkuu                   Ndugu Adam Alphonce Kivenule
4. Makamu Katibu Mkuu       Ndugu Vitus Nzala
5. Mweka Hazina                 Ndugu Justin Daniel Kivenule
6. Mweka Hazina Msaidizi     Ndugu Carolina Sigatambule Kivenule
7. Mweka Hazina Msaidizi     Ndugu Jermana Peter Mhapa
Sambamba na uchaguzi wa Viongozi wa KAUKI, mkutano uliwachagua Walezi wa Kanda na kubainisha majukumu yao.

Majukumu Makuu ya Walezi ni:
1.    Kuhamasisha Wana-KAUKI katika Kanda ili wawe na mwamko katika masuala mbalimbali yanayohusiana na maendeleo ya KAUKI. Kumekuwepo na kususua sua kwa shughuli za KAUKI katika Kanda iwepo kushindwa kubisa kutekelezwa kwa shughuli za maendeleo. Kuwepo kwa Walezi kutasaidia katika kuwahimiza viongozi waliopewa majukumu kuwajibika kikamilifu, na pia kuishauri jamii inayounda KAUKI katika maeneo hayo, kujitoa kwa hali na mali.

2.    Kuwahimiza viongozi kuwajibika kwa mujibu wa nafasi zao. Majukumu yote ya viongozi yapo katika Katiba ya KAUKI. Hivyo pale Ambato itaonekana uongozi unazembea, Mlezi wa Kanda ana jukumu la kuwahimiza viongozi husika kujiwabika kwa mujibu wa majukumu yake ya kazi.

3.    Kuhudhuria vikao vyote vya Kanda ambavyo vitaitishwa na Viongozi wa Kanda wa KAUKI au vile vya Kamati mbalimbali za KAUKI katika Kanda.

4.    Kuitisha kikao/vikao katika Kanda kama kuna suala la msingi ambalo linapaswa kuzunguzwa na kujadiliwa kwa maendeleo ya KAUKI.

Viongozi Walezi wa Kanda waliochaguliwa ni pamoja na:
1. Ndugu Innocent Samwel Kivenule (Kanda ya Dar es Salaam)
2. Ndugu Amalia Kivenule (Kanda ya Irore)
3. Ndugu Augustino Kivenule (Kanda ya Nduli)
4. Ndugu Happy Kivenule (Kanda ya Mufindi)
5. Ndugu Benard Kivenule (Kanda ya Magubike)
6. Ndugu Donath Peter Mhapa (Kanda ya Kidamali)

Wa kwanza kushoto, Mwenyekiti Mpya wa KAUKI aliyerejea tena madarakani, kuongoza KAUKI kwa kipindi cha miaka 3.
Mkutano Mkuu wa 9 wa KAUKI uliwaelekeza wajumbe wa Mkutano huo kwenda kuwachagua viongozi wa Kanda katika Kanda zao.

Sambamba na yote hayo kufanyika, Mkutano Mkuu wa 9 wa KAUKI ulitangaza tarehe ya Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI kuwa ni tarehe 28 - 29 Juni 2014; utakaofanyika katika Kijiji cha Kidamali, Mkoani Iringa.

Imeandaliwa na:

Adam A. Kivenule
Katibu Mkuu - KAUKI
+255 713 270364