MKUTANO MKUU WA 10 WA KAUKI

MKUTANO MKUU WA 10 WA KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

KAUKI-Kidamali, Iringa

KAUKI-Kidamali, Iringa
Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Friday, May 10, 2013

TATHMINI YA KAUKI KUELEKEA MKUTANO MKUU WA 9 WA KAUKI, 2013

Kuelekea Mkutano Mkuu wa 9 wa Umoja wa Ukoo wa Kivenule (KAUKI), kama mtendaji Mkuu wa umoja huu, ninakuja na tathmini ifuatayo:
  • Hatukufahamiana miongoni mwetu, 
  • Hatukuwa karibu kama ilivyo sasa, 
  • Hatukushirikiana baina yetu kama inavyofanyika sasa katika shida na raha,
  • Hatukutembeleana majumbani mwetu kama inavyofanyika leo hii.

Kwa muda wa miaka 8 ya KAUKI, tunashuhudia yafuatayo:
  1. Undugu, ushirikiano na mahusiano baina yetu yameboreka vilivyo:
  2. Tumefahamiana kama wana-ukoo na ndugu kutoka maeneo ya Irore, Nduli, Itagutwa, Mgongo, Igominyi, Isimani, Iringa Mjini, Kalenga, Kalenga, Nzihi, Kipera, Kidamali, Magubike, Nyamihuu, Idete, Ibogo, Nyamahana, Ipogolo, Mufindi, Dar na Morogoro;
  3. Kila mwaka tuna uhakika wa kukutana, kupongezana na kufarijiana kutokana na matukio mengi ya kijamii yaliyotokea katika jamii yetu;
  4. Hamasa na wahamasishaji wa kujitolea wapo na wenye moyo wa kujituma.

Tuiunge mkono KAUKI kwa nguvu zote ili isife, kwa kutoa michango na kushiriki Mkutano Mkuu wa 9 wa KAUKI, Kidamali - Iringa.

Imeandaliwa na kutolewa na:



KAUKI
Kanda ya Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment