MKUTANO MKUU WA 10 WA KAUKI

MKUTANO MKUU WA 10 WA KAUKI
Tangazo la Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

KAUKI-Kidamali, Iringa

KAUKI-Kidamali, Iringa
Mkutano Mkuu wa 10 wa KAUKI

Thursday, April 11, 2013

MKUTANO MKUU WA KWANZA WA UKOO WA KIVENULE: DESEMBA 17 – 18, 2005



Utangulizi
Harakati endelevu za kuleta mabadiliko na maendeleo zinavyokua kwa kasi kubwa na hivyo kuchochea mabadiliko ya haraka ya hali bora za maisha ulimwenguni. Harakati hizo zinazotegemea sana kuwepo wa sayansi na kiteknolojia na uchumi endelevu; zinatoa fursa na hamasa kwa jamii huria nazo kubuni na kutafuta mbinu mbadala za kuweza kujiinua ili kuweza kukabiliana na hali hiyo. Mabadiliko hayo ninayoyazungumzia ni pamoja na kukua kwa teknolojia ya habari na mawasiliano (computer, Internet na cellphones), soko huria, utandawazi na ubinafsishaji.

Jamii huria kwa upande wake zinapata hamasa na changamoto ya kuweza kutafuta mustakali wake kutokana na hali halisi ya maendeleo inavyoendelea kukua na athari kuonekana kwa upande mmoja na pia mafanikio kuonekana kwa upande mwingine.

Wimbi la umaskini uliokithiri, janga la UKIMWI, ujinga na rushwa vimekuwa ni vikwazo vikubwa vya maendeleo na ambavyo vinazidi kudidimiza harakati mbalimbali za kuweza kujiinua na kujikwamua katika hali hiyo. Harakati hizi za kutafuta maendeleo zimegawanyika katika makundi mbalimbali ya kijamii hususani makundi ya wasomi, wafanyabiashara, wanawake na wananchi wa kawaida.

Kutokana na harakati hizo, wanajamii wanaounda Ukoo wa Kivenule nao hawako nyuma katika kuhakikisha kuwa jamii yao inaondokana na umaskini, ujinga pamoja na UKIMWI; na hivyo kupata fursa ya kuishi katika dunia mbadala iliyojisheheneza katika sayansi na teknolojia.

Kwa kutambua hilo, wanajamii wanaounda Ukoo wa Kivenule, kwa pamoja toka mwezi Februari 06, 2005, walianzisha harakati za kuinasua jamii yao kutoka kwenye lindi la umaskini, ujinga na maradhi kwa kuunda Kamati Tatu kuratibu Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Ukoo huo; ambao umepangwa kufanyika katika Kijiji cha Kidamali, Wilaya ya Iringa Vijijini mkoani Iringa, hapo tarehe 17 hadi 18 Desemba 2005. Kwa kushirikisha Kamati Tatu za Maandalizi ya Mkutano Mkuu, yaani Kamati iliyopo mkoani Dar es Salaam, Kamati ya Kijijini Kidamali na ile ya Ilole – Iringa, zote zimepewa majukumu mazito ya kusaidia kufanikisha mkutano huo.

Mkutano Mkuu wa Ukoo unategemea kuwaalika ndugu na wageni wapatao mia mbili (200) toka Kijijini Kidamali, Ilole, Nduli, Kihesa, Ilula, Magubike, Kinyamlewa, Nzihi, Iringa Mjini, Kalenga, Ipogolo, Museke, Kitwilu, Igowolo, Kiponzelo, Mafinga, Mufindi, Maduma, Wasa, Ifunda, Tosamaganga, Tanangozi, Sadani, Isimani, Kilombero, Morogoro, Dodoma na Dar es Salaam; na sehemu nyingine nyingi ambako wanajamii wanaounda ukoo huo wanaishi ili waweze kupata fursa ya kushiriki kikamilifu.

Kamati hizo zikiwa chini ya viongozi wahamasishaji ambao ni:
1.        Adam Kivenule               Katibu – DAR                                   0741 270364/0748 270364
2.       Christian Kivenule                        Mwenyekiti – DAR                            0744 031 675
3.       Athuman Mtono             Makamu Mwenyekiti – DAR                      0748 708 708
4.       Edgar Kivenule                Mshauri wa Kamati – DAR  0748488523 / 0741215724
5.       Innocent Kivenule                        Mweka Hazina – DAR                     0748 663 315
6.       Ndugu Ignas Kivenule     (Mshauri Kamati ya Ilole);                0744 060 183
7.       Ndugu Faustin Kivenule Mwenyekiti (Kamati ya Kidamali) 
8.       Augen Kivenule               Makamu Mwenyekiti (Kamati ya Kidamali) 0748859936
9.       Jovin Kivenule                  Katibu (Kamati ya Kidamali)
10.   Carolina Kivenule                        Katibu Msaidizi (Kamati ya Kidamali)
11.      Justin Kivenule                 Mweka Hazina (Kamati ya Kidamali) 0748 855 739
12.    Donati Mhapa                 Mshauri (Kamati ya Kidamali)        0748 481 954

zimepewa jukumu la kuhakikisha kuwa Mkutano Mkuu unafanyika na kufanikiwa.

Ukoo wa Kivenule ukiwa umejiwekea malengo mahususi katika kuandaa mkutano huo, pia umeazimia pamoja na mambo mengine, kufundisha jamii inayounda ukoo huo kwa kutoa Mada Tano zenye msukumo wa maendeleo. Mada zilizopendekezwa kufundishwa katika siku mbili za mkutano ni pamoja na UKIMWI, ELIMU, MAHUSIANO BAINA YA WANANDUGU, KUKUA NA KUENEA KWA UKOO NA DINI.

Wawezeshaji mbalimbali wenye ujuzi katika mada hizo tayari kamati zimechukua jukumu la kuwatafuta ikiwamo kupata wataalam toka Tume ya UKIMWI ya Taifa (TACAIDS).

Mojawapo ya hamasa kubwa ya kuandaa mkutano huu ni pamoja na suala nzima la mahusiano ndani ya wanandugu, wanaukoo na jamii kwa ujumla. Suala la ELIMU, ATHARI ZA UKIMWI katika jamii ya ukoo wa Kivenule na taifa nzima kwa ujumla, haja ya kufahamiana baina ya wanajamii wanaounda ukoo, pamoja na kuujua ukoo kwa ujumla.

Pamoja na mambo mengine, kamati ilifikiria pia uwezekano wa kufanya senza ili kujua idadi ya ndugu wanaounda ukoo husika toka kona mbalimbali hapa Tanzania; kujua nini wanakifanya na kujua idadi sahihi ya wanandugu ambao wanahitaji msaada wa namna moja au nyingine.

Katika suala nzima la Kufahamu Chimbuko la Ukoo, Mahusiano baina ya wanandugu ndani ya ukoo, Elimu, Maadili na Dini na gonjwa hatari la UKIMWI, Kamati ilionelea kuwa ni mojawapo ya mambo msingi sana kuyaangalia katika shughuli nzima ya maandalizi na wakati wa Mkutano Mkuu.

Changamoto zitapatikana baada ya kuyagusia mambo haya ya msingi na hivyo kuwawezesha washiriki wa mkutano mkuu kujenga ajenda mpya.

Mahusiano duni baina ya wana ndugu, kukosa kwa ushirikiano katika mambo mbalimbali ya kimaendeleo, hali duni ya kiuchumi na kijamii, matatizo ya kifamilia na kiukoo ni kati ya masuala msingi yaliyofikiriwa sana kabla ya kuanza kufanya maandalizi ya Mkutano Mkuu.

Mwelekeo na nafasi ya ukoo wa Kivenule katika suala nzima la Elimu hasa katika dunia hii ya Utandawazi (Globalization). Maendeleo ya sayansi na teknolojia ambapo yameifanya dunia kuwa kama kijiji kisicho na mipaka na kila mtu anaruhusiwa kuingia na kutoka; kuongezeka kwa viwanda vinavyotumia teknolojia ya hali ya juu; kuongezeka kwa teknolojia ya habari na mawasiliano (Internet); kupanuka na kujengeka kwa miji, pamoja na soko huria.

Mambo yote haya ndiyo yanayoweza kuonyesha mustakabali na nafasi ya ukoo wa Kivenule kwa maisha ya baadaye. Ilionekana kuwa ukoo wetu upo nyuma sana katika suala nzima la elimu, hii linajidhihirisha kutokana na kuwa na ndugu wachache sana ambao wameweza kupata elimu kwa kiwango kinachostahili.

Hii ni hatari kwa sababu tunajenga ukoo tegemezi ambayo baadaye utakosa mwelekeo. Mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia yanayojitokeza kila kukicha yanaibadili dunia na hivyo kutulazimisha nasi katika ukoo wa Kivenule kubadilika. Matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano katika simu za mikononi, Internet, computer, redio na satelaiti ni changamoto kubwa katika Ukoo wa Kivenule.

Maambukizo ya ugonjwa wa UKIMWI ambayo kwa kiasi kikubwa yameathiri familia nyingi zikiwemo familia zetu sisi wana ukoo, yanapaswa kutopuuzwa bali kuwekewa mikakati madhubuti. Ufahamu kuhusiana na gonjwa lenyewe livyoenea na madhara yake katika jamii, njia mbadala za kujilinda na maambukizi ya ugonjwa wenyewe pamoja na kuitikia mialiko mbalimbali ya wanajamii wanaopambana na janga hili ni mambo ya msingi sana ambayo yatajadiliwa kwa kina kwenye mkutano huo.

Ilipendekezwa kuwa, wakati wa mkutano huo kutakuwa na nafasi kutoa uzoefu katika mambo mbalimbali ya kitaalum na maendeleo. Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Ukoo yalianza mapema ili kumpa fursa kila mwanajamii/mwanaukoo kutafakari na kujadili kwa kina, kujiandaa pamoja na kuwasilisha mchango wake wa mawazo kwa kamati husika za kuratibu maandalizi.

Mkutano Mkuu wa Ukoo umeazimia kutoa kitu muhimu ambacho ndicho kitakuwa mwongozo na dira ya shughuli mbalimbali zitakazokuwa zinafanyika katika ukoo.
Licha ya kuwa na malengo na makusudio mbalimbali, pia tunategemea mwisho wa mkutano kutakuwa na mambo kadhaa ambayo yatakuwa ni makubaliano kutoka pande mbalimbali za ukoo wa Kivenule. Yote hayo kwa pamoja yatakuwa ni maazimio ya Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo wa Kivenule.

Kati ya Maazimio ambayo tunayategemea katika mkutano huo ni:
  1. Kufanya Senza ya Ukoo wa Kivenule ili kupata idadi kamili ya ndugu.
  2. Kuanzisha Mfuko wa Ukoo
  3. Kuchagua Viongozi wa watakaounda Kamati ya Ukoo ya Kuratibu mambo mbalimbali ya ukoo. (Mwenyekiti, Katibu, Mweka Hazina pamoja na viongozi wengine ambayo wana umuhimu na kupewa majukumu kuwepo).
  4. Kuzitaja kazi mbalimbali ambazo Uongozi utakaoundwa utakuwa unazifanya mfano kufanya mashauriano na usuluhishi wa matatizo mbalimbali ya ukoo yaliyojitokeza.
  5. Kukusanya taarifa mbalimbali za ukoo; na
  6. Kuangalia na Kutathmini usalama wa mali mbalimbali zinazomilikiwa na ukoo nk.
Katika kuhakikisha kuwa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo unafanyika na kufanikiwa, kamati mbalimbali ndogondogo zinategemea kuundwa ili kusaidia uratibu maandalizi ya mkutano huoo kabla ya kuanza na wakati wa mkutano huo. Mojawapo wa kamati hizo ni: Kamati ya Mapokezi; Kamati ya Malazi; Kamati ya Chakula; Kamati ya Vinywaji; Kamati ya Burudani; Kamati ya Usafiri; Kamati ya Ulinzi na Usalama; Huduma ya Kwanza na Kamati ya Uratibu wa Shughuli za Mkutano.

Kwa kushirikiana na Kamati Kubwa (ile iliyoundwa Dar es Salaam, ya Kidamale na ile ya Ilole) katika kuratibu maandalizi ya Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo, kamati ndogondogo zitajumuika kutekeleza majukumu mbalimbali kabla na siku ya Mkutano Mkuu wa Ukoo wa Kivenule. Kwa hiyo Kamati zote kwa pamoja zitakuwa na wajibu wa kufanya yafuatayo ili kuhakikisha shughuli nzima inaenda kama ilivyopangwa. Mojawapo ya majukumu hayo ni pamoja na:-

·         Kuoganaizi (kuandaa) huduma ya usafiri toka Iringa Mjini hadi Kidamali kwa wageni mbalimbali ambao watakuwa wanakuja kwenye Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Ukoo; huo pamoja na kuandaa orodha ya wageni na tarehe zao kufika Kidamale. Hii itakusaidia sana kwenye zoezi zima la kuoganaizi huduma ya usafiri kwa wageni mbalimbali ambao wengi wao watakuwa hawapajui vizuri kidamali.

·         Kufanya matayarisho ya sehemu ya Malazi kwa wageni mbalimbali ambao watawasili kutoka sehemu mbalimbali. Hii inajumuisha sehemu salama na nadhifu za kulala wageni husika ambapo tunategemea tutapata vyumba, magodoro pamoja na kuwepo kwa vyoo na mabafu ya kuogea.

·         Kuhakikisha kuwa shughuli zote zinazohusiana na maandalizi ya vyakula zimepangiliwa vizuri. Kula chakula katika muda uliopangwa, huduma ya chai/kahawa na maji wakati mkutano unaendelea viende kama ratiba itakavyokuwa imepangwa. Hii inamaanisha kuwa, RATIBA pamoja na matangazo mbalimbali  yatabandikwa sehemu mbali kwenye eneo la mkutano (ukumbi), jikoni, maeneo mbalimbali ya Kijiji cha Kidamali. Hii itasaidia kuwafanya washiriki wa mkutano kujali na kuona umuhimu wa mkutano.

·         Kutaundwa kamati ndogo ndogo zenye wajibu wa kutekeleza majukumu zitakazopangiwa na kamati kubwa. Mfano wa kamati hizo ndogo ni pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama, Kamati ya Usafi, Kamati ya Chakula, Kamati ya Vinywaji, Kamati ya Malazi, Kamati ya Mapambo, Kamati ya Picha za Video na Picha za Kawaida na Kamati ya Burudani. Kamati zote hizo ndogo ni muhimu sana kwani ndizo zitakazosaidia shughuli nzima kwenda kama ilivyokusudiwa.

·         Lazima uwepo usimamizi madhubuti ili kuwezesha shughuli mbalimbali kuwa ndani ya ratiba (muda uliopangwa). Kwa hiyo kuna haja ya kuwepo kwa saa za ukutani ambazo zitakuwa kama mwongozo. Hii tunamaanisha kuwa Wawezashaji lazima wawe wachangamfu sana wakati wa kuendesha mada mbalimbali pamoja na majadiliano.

·         Kazi nyingine kubwa ni kuhamasisha wanakoo mbalimbali wanaishi ndani ya Kidamali na kwingineko kuwa na moyo wa kujitolea katika shughuli mbalimbali zitakazojitokeza kwenye mkutano. Hii ni pamoja na kuzisaidia kamati ambazo zitaonyesha hali ya kuelemewa au kuhitaji msaada wa kiutendaji.

Baadhi ya wawezeshaji waliopendekezwa toka katika ukoo husika ni pamoja na:
1.        Agatha                 Mhapa
2.       Alphonce              Kivenule
3.       Lizeta                   Kivenule
4.       Ignas                     Kivenule
5.       Siha                      Kivenule
6.       Christian               Kivenule
7.       Adam                   Kivenule
8.       Justin                     Kivenule
9.       Donath                 Mhapa
10.   John                      Kivenule
11.      Victoria                 Kivenule
12.    Edger                    Kivenule
13.    Piera                     Kivenule
14.    Florian                  Kivenule
15.    Innocent               Kivenule
16.    Stephen                Mhapa
17.     Severin                 Nyangalima

Mada zitakazowasilishwa kwenye mkutano mkuu ni pamoja na

1.      CHIMBUKO NA HISTORIA YA UKOO
  • Ukoo ni Nini na Unapatikanaje?
  • Dhana ya Kuenea na Kukua kwa Ukoo.
  • Mgawanyiko wa Ukoo (Chora Mchoro Kuonyesha Ukoo unavyoundwa).
  • Kupotea kwa Ukoo.
2.     MAHUSIANO BAINA YA NDUGU NDANI YA UKOO
  • Ukaribu wa Wana Ndugu.
  • Ushirikiano Katika Nyanja Mbalimbali.
  • Kutembeleana kama Sehemu ya Kudumisha Mahusiano.
  • Kuondoa Tofauti na Kusaidiana.

3.   ELIMU NA MUSTAKABALI WA UKOO
  • Nafasi ya Ukoo wa Kivenule katika Elimu.
  • Umuhimu wa Elimu.
  • Dunia ya Utandawazi.
  • Nini Kifanyike Kuinua Elimu Katika Ukoo Wetu.

4.   UKIMWI NDANI YA UKOO NA ATHARI ZAKE
  • UKIMWI ni nini?
  • Namna gani UKIMWI unavyoenea/kuambukizwa?
  • Njia Mbadala za Kujilinda na Maambukizi?
  • Jukumu la Ukoo/Familia Kukabiliana na Janga la UKIMWI.
                         
5. DINI KATIKA UKOO
  • Maana ya Dini
  • Umuhimu wa Kuwa na Imani
  • Maadili na Dini
  • Ukoo Uliojengeka katika Misingi ya Dini

RATIBA YA MKUTANO MKUU WA KWANZA WA UKOO WA KIVENULE

Siku ya Kwanza ya Mkutano Mkuu wa Ukoo wa KIVENULE

Muda na tarehe
17 Des. 2005
Shughuli/Jukumu
Wahusika
12:00–12:45
Wageni Wote Kuamka na Kufanya Maandalizi ya Kuingia kwenye Mkutano

Wote

12:45–1:45
Kupata Kifungua Kinywa
Wote
1:45 – 2:45
Kuwasili Mkutanoni na Kujisajili
Wote
2:45 – 3:15
Ufunguzi wa Mkutano na Mgeni Rasmi
Mgeni Rasmi
3:15 – 4:00
Utambulisho baina wa wana Ndugu
Wote
4:00 – 4:45
Pumziko la Chai / Kahawa/Maji
Wote
4:45 – 5:30

Mada ya Kwanza: CHIMBUKO NA HISTORIA YA UKOO

Mtoa Mada na Mkubwa wa Ukoo

5:30 – 6:00
Majadiliano katika Makundi
Makundi 4
6:00 – 6:20
Murejesho na Majumuisho
Mwezeshaji
6:30 – 8:00
CHAKULA CHA MCHANA
Wote
8:00 – 8:45
Mada ya Pili: MAHUSIANO BAINA YA NDUGU NDANI YA UKOO WA KIVENULE
Mtoa MADA (…………………)
8:45 – 9:15
Majadiliano katika Makundi
Makundi 4
9:15 – 9:45
Murejesho na Majumuisho
Mwezeshaji
9:45– 10:45

Pumziko la Chai/Kahawa/Maji

Wote
10:45-1:30 Usiku
Mapumziko Marefu (Kusalimiana na Kufahamiana zaidi)
Ndugu na Wageni Wote
1:30 – 2:30
Chakula cha Usiku na Vinjwaji
Ndugu Wote
2:30 – 6:30
Burudani (Muziki wa Kisasa na Ngoma za Asili)
Wote

Siku ya Pili ya Mkutano Mkuu wa Ukoo wa KIVENULE

Muda
18 Des. 2005
Shughuli/Jukumu
Wahusika
12:00– 12:45
Kuamuka na Kufanya Maandalizi ya Mkutano

Wote

12:45 – 1:45
Kifungua Kinywa
Wote
1:45 – 2:15
Kuwasili Mkutanoni na Kujisajili

Ndugu wote

2:15 – 2:45
Mada Ya Tatu: ELIMU NA MUSTAKABILI WA UKOO WA KIVENULE

Mtoa Mada

2:45 – 3:15
Majadiliano kwenye Makundi
Makundi 4
3:15 – 3:45
Murejesho na Majumuisho
Kiongozi wa Kundi na Mwezeshaji
3:45 – 4:30
Pumziko la Chai/Kahawa/Maji
Wote
4:30 – 5:00

Mada ya Nne: UKIMWI NDANI YA UKOO NA ATHARI ZAKE

Mtoa Mada

5:00 – 5:30

Majadiliano kwenye Makundi

Makundi 4

5:30 – 6:00

Murejesho na Majumuisho

Kiongozi wa Kundi na Mwezeshaji

6:00 – 7:15
CHAKULA CHA MCHANA

Wote

7:15 – 7:45

Mada ya Tano: DINI KATIKA UKOO

Mtoa Mada

7:45 – 8:15

Majadiliano kwenye Makundi

Makundi 4

8:15 – 8:45

Murejesho na Majumuisho

 

8:45 – 9:45

Majumuisho:

1.      Yote Yaliyojitokeza

2.     Matarajio

3.     Tarehe ya Mkutano Mwingine

Mwezeshaji

9:45 – 10:15
Shukurani toka kwa Ndugu Mbalimbali
Mgeni Rasmi, Ndugu
10:15–11:00
KUCHAGUA VIONGOZI WA KUUNDA KAMATI YA UKOO
Ndugu Wote
11:00
Kufunga Mkutano
Viongozi wa Kamati ya Ukoo

No comments:

Post a Comment